Tuesday, May 14, 2013

Wafugaji wa nyuki wa Wilaya ya Hanang’ Mkoani Manyara wametakiwa kutumia fursa za soko la asali toka kampuni ya Honey King ya mjini Kibaha mkoani Pwani kwa kujinyanyua kiuchumi.


Hayo yalisemwa jana tarehe 04/04/2013 na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji na Uwezeshaji) Dk Mary Nagu ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Hanang’ kwenye uhamasishaji wa vikundi vya ujasiriamali wa ufugaji wa nyuki wilaya ya Hanang. Dk Nagu alisema vikundi 13 kupitia vyama vyao vya kuweka na kukopa (Saccos) wataweza kujinufaisha kimaendeleo kwa kujiwezesha kiuchumi pindi wakitumia fursa hiyo ya kuwepo na soko la uhakika la asali kupitia Honey King. Alisema wadau hao wa ufugaji wa nyuki wanatakiwa kujipanga,kwani shughuli za ufugaji wa nyuki hazihitaji gharama kubwa na pia soko la asali siyo tatizo tena kwani halihitaji kutafutwa lipo karibu na kwa uhakika. Aliwataka vijana wengi zaidi wa wilaya hiyo kujiunga kwenye vikundi na kuchangamkia fursa hiyo kwa kufuga nyuki,ambazo zitawapatia asali ya kutosha na kuondokana na umasikini kwenye jamii zao. Naye,Mratibu wa kampuni ya Honey King Filbert Sanka,alisema soko lao lina uwezo wa kununua tani 300 za asali hivyo wajasiriamali wa wilaya hiyo waitumie kwa kuhakisha wanakusanya asali ya kutosha na kuwauzia

No comments:

Post a Comment