WAZIRI MKUU Mizengo Pinda ametunukiwa Tuzo ya Heshima ya Mwaka 2012 ya Mkoa wa
Katavi katika vipengele viwili vya Utawala Bora na Uhamasishaji wa ufugaji
nyuki.
Waziri Mkuu alipokea tuzo hizo, kwenye hafla ya
kuuaga mwaka 2012 na kuukaribisha mwaka 2013 iliyofanyika kwenye ukumbi wa
Idara ya Maji mjini Mpanda,
Akitoa maelezo ya utangulizi kabla ya kutangaza
majina ya watunukiwa, Katibu Tawala wa Mkoa wa Katavi, Mhandisi Emmanuel
Kalobelo alisema mkoa wa Katavi umeamua kuanzisha mfumo wa utoaji wa Tuzo ya
Mkoa kwa lengo la kuwatambua, kuwatia moyo na kuwapa motisha wananchi na
watumishi wa umma waliofanya vizuri katika nyanja mbalimbali za utoaji wa
huduma kwa wananchi.
Sekta
zilizopewa tuzo ni mapato na kodi za Serikali, utawala bora, uchumi na
maendeleo, Ulinzi na usalama, mipango miji, mawasiliano na teknolojia, ufugaji
nyuki na hifadhi ya mazingira, elimu, kilimo na mifugo, michezo, usafirishaji
na huduma za jamii.
Waziri
Mkuu Mizengo Pinda anatunukiwa tuzo ya utawala bora, siasa safi na ushiriki
katika shughuli za maendeleo ya wananchi wa jimbo lake la Katavi na Ukanda wa
Ziwa Tanganyika kikamilifu.
Mhandisi
Kalobelo amesema Tuzo hiyo itaendelea
kutolewa kila mwisho wa mwaka ambapo wameamu kufanya hivyo ili kuamsha ari kwa wengine kufanya vizuri
zaidi mwaka unaofuata.
No comments:
Post a Comment