Thursday, February 7, 2013

PINDA ATUNUKIWA TUZO YA HESHIMA BORA NA UFUGAJI WA NYUKI 2012




WAZIRI MKUU Mizengo Pinda ametunukiwa  Tuzo ya Heshima ya Mwaka 2012 ya Mkoa wa Katavi katika vipengele viwili vya Utawala Bora na Uhamasishaji wa ufugaji nyuki.

Waziri Mkuu alipokea tuzo hizo, kwenye hafla ya kuuaga mwaka 2012 na kuukaribisha mwaka 2013 iliyofanyika kwenye ukumbi wa Idara ya Maji mjini Mpanda,
Akitoa maelezo ya utangulizi kabla ya kutangaza majina ya watunukiwa, Katibu Tawala wa Mkoa wa Katavi, Mhandisi Emmanuel Kalobelo alisema mkoa wa Katavi umeamua kuanzisha mfumo wa utoaji wa Tuzo ya Mkoa kwa lengo la kuwatambua, kuwatia moyo na kuwapa motisha wananchi na watumishi wa umma waliofanya vizuri katika nyanja mbalimbali za utoaji wa huduma kwa wananchi.
  
Sekta zilizopewa tuzo ni mapato na kodi za Serikali, utawala bora, uchumi na maendeleo, Ulinzi na usalama, mipango miji, mawasiliano na teknolojia, ufugaji nyuki na hifadhi ya mazingira, elimu, kilimo na mifugo, michezo, usafirishaji na huduma za jamii.

Waziri Mkuu Mizengo Pinda anatunukiwa tuzo ya utawala bora, siasa safi na ushiriki katika shughuli za maendeleo ya wananchi wa jimbo lake la Katavi na Ukanda wa Ziwa Tanganyika kikamilifu.

 Mhandisi Kalobelo amesema Tuzo hiyo  itaendelea kutolewa kila mwisho wa mwaka ambapo wameamu kufanya hivyo  ili kuamsha ari kwa wengine kufanya vizuri zaidi mwaka unaofuata.


No comments:

Post a Comment