Kwa
kawaida makundi ya nyuki katika nchi ya Tanzania na baadhi ya nchi
zinazolingana kwa tabia za nchi, makundi ya nyuki huanza kutafuta sehemu salama
na yenye chakula kwa wingi kuanzia mwezi wa kumi katika mwaka mpaka mwezi wa
nne kwa mwaka unaofuata.Kipindi hiki huwa na makundi mengi yanayozunguka hapa
na pale kutafuta nyumba ambayo itawafaa kwa ajili ya makazi yao na kwa ajili ya
kuhifadhia chakula.
Hiki
ndio huwa kipindi muafaka sana kwa wafugaji kuanza kutega mizinga ambayo
imeshaandaliwa kwa ajili ya kufugia nyuki.Kwa kuwa makundi mengi huwa
yanatafuta sehemu za makazi hivyo ni rahisi sana kuyakama na kuyahifadhi
makundi hayo kwa ajili ya uzalishaji wa mazao ya nyuki.
Kutokana
na hilo, mfugaji anapaswa kuanza kuandaa sehemu ya kufugiua nyuki na mizinga
yake mapema zaidi kabla ya msimu huo kufika ili asiweze kukosa makundi ya
nyuki.Unashauriwa kuanza kuandaa mazingira ya kufugia nyuki na mizinga angalau
mwezi mmoja kabla kwa kusafisha, kukarabati au kutengeneza kile unachokihitaji.
VIFAA VINAVYOPASWA KUANDALIWA.
Kabla ya kuanza kufuga nyuki kuna vifaa ambavyo mfugaji wanyukiu anapaswa kuanza kuviandaa mapema kabla ya msimu wa ufugaji wa nyuki kufika.Vifaa hivyo ni kama vifuatavyo:-
UJENZI WA MABANDA YA KUFUGIA NYUKI.
Eneo
ambalo kuna wanyama wa aina mbalimbali ambao wanaweza kufanya uharibifu
mbalimbali wa mizinga pindi ikiwa na nyuki na kusababisha uharibifu wa mizinga,
kuua nyuki au hata mnyama mwenyewe kufa kutokana na kudungwa na nyuki.Hivyo
ujenzi wa mabanda ya kufugia nyuki ni vyema ukafanyika.
DHAMIRA YA UJENZI WA MABANDA YA KUFUGIA
NYUKI.
Mabanda
hayo ya kufugia nyuki yanaweza kuwa ya udongo, tofali au ya miti pekee pande
zote, milango pamoja na kuezekwa kwa nyasi.
Kuna
sababu mbalimbali ambazo zinasababisha mfugaji nyuki kuweza kujenga mabanda ya
kufugia nyuki, miongoni mwa sababu hizo ni:-
1.
Kukinga mizinga na jua na mvua.
Hii ni
sababu moja wapo ambayo inasababisha mfugaji wa nyuki kuamua kujenga mabanda ya
kufugia nyuki, mzinga unapokuwa kwenye kivuli huusaidia mzinga kuweza kudumu
kwa kipindi kirefu, pia kivuli husaidia nyuki kufanya kazi zao kwa juhudi.Iwapo
mzinga utakuwa upo kwenye jua nyuki hutumia muda mwingi kupunguza joto la ndani
ya mzinga badala kutumia muda huo kwa ajili ya kutafuta chakula.
Nyuki
wanapoona jua ni kali zaidi na kusababisha joto kali ndani ya mzinga huamua
kuhama katika mzinga huo na kwenda kutafuta makazi sehemu nyingine.Hivyo nio
vyema mzinga ukakaa kwenye kivuli na sehemu isiyoweza kunyeshewa na mvua.
Pia
mvua inaponyeshea mzinga husababisha mbao kuweza kuoza ndani ya muda mfupi,
hivyo kwa kujengea banda la kufugia nyuki huweza kuukinga mzinga wako dhidi ya
mvua ambayo inasababisha kuozesha mbao za mzinga wako.
2.
Kukinga na wanyama waharibifu
Mabanda
haya ya kufugia nyuki husaidia sana kwa wanyama waharibifu wa mizinga kushindwa
kuifikia mizinga lakini pia husaidia sana kupunguza mashambulizi ya nyuki kwa
viumbe wengine.Mizinga huwekwa ndani ya banda na banda kufungwa milango.
3.
Ulinzi na ukaguaji
Ujenzi
wa mabanda ya kufugia nyuki husaidia sana kuiweka mizinga yako sehemu salama
dhidi ya wezi wa mizinga au asali lakini pia husaidia sana wakati wa uangalizi
wa mzinga.Mizinga inapokuwa pamoja uangalizi wa mizinga hiyo huwa ni rahisi
sana na pia huweza kusaidia kipindi cha uvunaji na uwekaji wa kumbukumbu za
kila mara.
Pembeni
ya banda hilo sehemu ambazo mizinga inawekwa huwekwa matundu maalumu ya kutoka
na kuingia nyuki kwa ajili ya kujitafutia chakula chao.
MIZINGA YA KUFUGIA NYUKI.
Mizinga
ya kufugia nyuki inapaswa kuandaliwa mapema kabla ya msimu wa kukamata makundi
ya nyuki haujafika.Mizinga inayopaswa kuandaliwa ni kama ifuatayo:-
1.
Mzinga wa kibiashara
Huu ni
mzinga wa kisasa unaotumika kwa wafugaji wa nyuki hasa wale wanaotaka kuvuna
asali kwa wingi kwa ajili ya kuuza.Mzinga huu huweza kuzalisha asali kwa wingi
kadri misimu ya uvunaji inavyoongezeka mwaka hadi mwaka.
Mzinga
huu una sehemu kuu tatu kama zifuatazo:-
a.
Box la kuzalishia watoto wa nyuki
Ni box
ambalo kwa kawaida huwa la kwanza kwa upande wa chini.box hili ndilo ambalo
huwa na mlandfo wa nyuki kuingia na kutoka pindi wanapokwenda na kutoka kwenye
utafutaji wa chakula.Box hili hutumika na malikia wa nyuki kwa kutagia mayai
pamoja na kulelea watoto ambao husubiri kuanguliwa na kuwa nyuki kamili.
Pia box
hili hutumika kwa ajili ya nyuki kuhifadhia chakula chao kwa ajili ya msimu wa
kiangazi, msimu ambao huwa hauna maua yenye chakula cha nyuki cha kutosha,Hivyo
mfugaji hapaswi kuvuna asali anayoikuta katika brood box, kwa kuvuna asali
unayoikuta katika brood box husababisha kundi lako kuhama kwa kukosa chakula.
Kwa
kawaida matumizi ya mzinga huu huanza kuvuna asali baada ya wastani wa misimu
miwili mikubwa yaani sawa na miaka miwili.Na mara baada ya kipindi hicho kipita
mfugaji huweza kuanza kuvuna kwa vipindi tofauti tofauti vya mwaka na
kuendelea.
b.
Kitenga malikia
Hiki ni
kifaa kama nyavu ambacho huwekwa kati ya brood box na super box, wavu huu
huweza kumzuia malikia asiweze kupanda katika super box kwa lengo la kutaga
mayai.matundu ya waya huu ni madogo kulingana na umbile la nyuki watenda kazi
peke yao.Hivyo malikia na madume ya nyuki hayawezi kupanda kuelekea kwenye
super box.
c.
Box la kuhifadhia asali
Hili ni
box ambalo huwekwa juu mara tu baada ya queen excluder.Box hili huwa ni maalumu
kwa nyuki watenda kazi kuweza kuhifadhi asali yao kwa wingi.Asali inayokuwa
katika box hili haiwezi kuchanganyika na watoto wa nyuki wala chavua kutokana
na kuwapo kwa queen excluder chini yake.Asali inayotoka katika Box hili huwa
nzuri na safi kutokana na kutochanganyika na masega ambayo yalitumika kwa
kuangulia watoto wa nyuki.
Uvinaji
wa asali katika mzinga huu, mfugaji anapaswa kutoa frame zilizopo katika super box
ambazo asali yake tayari imeiva.Mara baada ya kutoa frame hizo mfugaji anapaswa
kukamua asali hiyo kwa kutumia mashine ya kisasa iitwayo Honey Centrifuge Machine.Mashine hii huweza
kufyonza asali yote iliyopo katika sega na kubakiza sega likiwa halina asali.
Mara
baada ya hapo mfugaji anapaswa kurudisha sega hilo kwenye mzinga likiwa na
frame yake ili nyuki aweze kujaza asali tena.Hii inamsaidia sana nyuki
kumpunguzia kazi ya kujenga sega jipya la Sali kila baada ya mvuno wa asali na
hivyo kuongeza uzalishaji wa asali mara dufu.Tofauti tu ya aina ya mzinga huu
ni kwamba huwezi kupata zao la nta.
2. Mzinga wa viunzi
Huu ni
mzinga wa teknolojia ya kati kutoka kwenye mizinga ya kienyeji na kuelekea
mizinga ya kisasa.Mzinga huu uhifadhi wake wa asali hautofautiani sana na
uhifadhi wa asali katika mizinga ya kienyeji, isipokuwa katika mzinga huu
masega hupangwa kwa kufuata utaratibu wa viunzi vilivyowekwa.nyuki huweka sega
moja katika kila kiunzi kimoja cha mzinga huu.
Mzinga
huu pia haujagawanywa kwa kutenganisha sehemu za kuhifadhia asali na sehemu ya
malikia kuangulia watoto.Hivyo asali itokayo katika mzinga huu huweza
kuchanyanyika na watoto iwapo mfugaji hatakuwa makini katika uvunaji wa asali
hiyo.
Uvunaji
wa mzinga huu, mfugaji anapaswa kukata sega lote lenye asali pekee na
kulihifadhi katika chombo kisafi kwa jili ya kukamua asali hiyo kwa kutumia
mashine ya kusasa au kwa kutumia njia za kitamaduni.
PICHA ZA MABANDA TOFAUTI TOFAUTI YA KUFUGIA NYUKI
Picha 2:Banda la kufugia nyuki lililojengwa kwa miti na kuezekwa kwa nyasi
Picha 3:Nyumba ya kufugia nyuki iliyojengwa kwa matofali na kuwekewa midomo maalumu ya nyuki kwa ajili ya kuingia na kutoka pindi wanapokwenda kutafuta chakula
Picha 4:Kibanda kidogo cha kisasa kwa jili ya kufugia nyuki.
Picha 5:Banda la kufugia nyuki lilijengwa kwa miti na kuezekwa kwa bati
Picha 6: Banda la kufugia nyuki lilijengwa kwa miti, kuezekwa kwa bati na kuwekewa uzio wa waya.
Hongera kwa maelezo mahsusi. Naomba kupata kitabu cha Ufugaji wa Nyuki.
ReplyDeleteMchg.Joseph Muhehwa
0756 025 146 / 0789 025 146
This comment has been removed by the author.
ReplyDeleteTunashukuru kwa kazii nzuri muliofanya ila naomba munitumie kitabu cha ufugaji wa nyuki.
ReplyDeleteAsante,
HUSSEIN AHMED
hirsitz@hotmail.com
naomba kupata kitabu cha ufugaji wa nyuki
ReplyDelete0654517602
ndichihero@gmail.com
dar es salaam
asanteni sana ndugu kwa elimu yen nzuri sana. Endeleeni kuielimisha jamii ili ijikwamue kiuchumi.
ReplyDeleteAhsante kwa maelezo, ila naomba kujua nia wapi ntapata mavaziya kuvunia asali?
ReplyDeleteUnaweza kupata mavazi kutoka kwetu lakini pia yapo makampuni binafsi ambayo pia unaweza kupata mavazi hayo, bei na ubora ni vitu unapaswa kuzingatia sana kabla ya kufikia hatua ya kununua vazi hilo
Deletenashukuru sana naomba kupata ratiba yenu kwa vipindi vya ufugaji wa nyuki
ReplyDeleteAsante sana Frolian kwa kutembelea ukurasa wetu, naomba ufahamu kuwa ratiba ya ufugaji nyuki zinatofautiana sana kulinga na eneo la nyuki walipo. Kwa mfano kwa sasa tuna mradi wetu Mkoani Tabora, ambapo vipindi vya ufugaji nyuki wa mkoa huu ni viwili yaani Msimu mkubwa unaonza mwezi June - August na Msimu mdogo unaonza mwezi Decemba - Februari. Ni vyema ukatufahamisha wewe kwa sasa unaishi mkoa gani
ReplyDeleteSamahan mfano kwa mkoa wa njombe je?
ReplyDeleteSamahan mfano kwa mkoa wa njombe je?
ReplyDeleteMa Vihe. Hbr naomba kuwasiliana na nyie mie nipo Tabora na ni mfugaji ila sina uzoefu
ReplyDeleteSamahani naomba kuwasiliana na nyie Mimi ni kijana ninayetaka kujikita katika suala LA ufugaji Wa nyuki nipo Sokoine university hapa morogoro
ReplyDeletenawezaje pata Kitabu cha ufugaji Nyuki?
ReplyDeleteMnapatikana wapi....kama kuna kitabu ngependa kukisoma email yangu ni fai.nargis@gmail.com
ReplyDeleteAhsante sana kwa makala hii kwa imekuwa chachu kwangu juu ya uanzzishaji wa kufuga nyuki mahali ninapoishi.
ReplyDeleteNaomba kupata kitabu cha namna ufugaji wa nyuki 0655071992
ReplyDeleteMimi naitaji nta Kama tan 1 je naweza kupata
ReplyDeleteutapata nicheki kwa number 0756428695
DeleteNmejifunza nashukuru sana kwa kupata elimu hii ntakapopata wasaha ntawasiliana nanyi
ReplyDeleteElimu ni nzuri Kikubwa ni kutoa hamasa zaidi ili kufikia hatua kubwa ya ufugaji
ReplyDeleteNilikua nahitaji vifaa vya kuvunia asali
ReplyDeleteNahitaji kujua ivunajinsumu ya nyuki na soko.make likoje?
ReplyDeleteSomo Zuri, Lakini Je Endapo Mtu Una Eneo Lililo Karibu Na Makazi Ya Watu Laweza Kufaa?
ReplyDeleteSomo zuri sana je naweza fuga nyuki ninapoishi bila madharaà
ReplyDeleteNashukuru kwa elimu nzuri nahitaji kujua bei ya mzinga mmoja wa kisasa na mavazi ya kuvaa unapowahudumia nyuki tafadhali.
ReplyDeleteNingeomba kitabu kama kipo au softcopy
ReplyDeleteAsanteni kwa darasa huru, natarajia kufanya mradi huu kwa ajili ya biashara. Hivyo Napenda kujua tathmini ya gharama za awali. Eneo lengwa Ni mkoani Tabora
ReplyDeleteKitabu tupate vip
DeleteShukran kwa elimu nzuri kuhusu ufugaji wa nyuki. Nataka kujua kama ufugaji huu unaweza kufanyika mikoa mingine zaidi ya Tabora. Mimi eneo langu liko mkoa wa Pwani ambako nataka kufanya mradi huu kibiashara. Pia nataka kujua gharama za mizinga ya kibiashara ili niweze kujipanga kuanza zoezi. Ahsante
ReplyDeleteNashukuru sana kwa elimu ya ufugaji nyuki.Mimi ni mfugaji wa nyuki nimeanza na mizinga ishirini ya kisasa,ninafuga eneo la Monduli juu Arusha nimeanza mwezi wa Dec mwaka jana 2019,natamani angalau kuwa na mizinga mia,ninaomba kujua ni wapi ninaweza kuuza asali kwa faida
ReplyDeleteNaomba msaada wenu wa hali na Mali Mimi nikijana ambae nahitaji sana na natamani sana kufuga nyuki ila ninaupungufu wa elimu ya nyuki kwa Sasa nipo chuoni ila napenda kujishungulisha na ufugaj wa nyuki kwa mda huu no 0622095530.msaada wenu wakuu.
ReplyDeleteElimu nzuri sanaaa
ReplyDeleteAsante sana kwa elimu safi. Mimi nataka kuuliza ni maeneo yapi na muhimu kwa ufugaji na pia kuhusu masoko yakoje?
ReplyDeleteAsante.Mimi naomba msaada wenu kufahamu kuhusu aina ya nyuki safi,gharama na masoko pia na bei za asali: Mathew 0787110812
ReplyDeletenataka nijue ni aina gani ya mimea ambayo nikiipanda itakuwa chakula cha nyuki
ReplyDeleteBlog nzuri sana
ReplyDeleteKwa mtu anayehitaji eneo la kufugia nyuki mnamsaidiaje?
ReplyDeleteAhsante sana ni mafunzo mazuri sana kwa mwenye nia ya kufuga nyuki kwa matumizi ya kawaida na kibiashara pia.
ReplyDeleteKwakweli nimependa elimu yenu je mtu akitaka kujifunza zaidi huwa mnadarasa?pia naweza kukipata kitabu?mimi samson toka arusha0786912960 samsnsanya127@gmail.com
ReplyDeleteKwakweli nimependa elimu yenu je mtu akitaka kujifunza zaidi huwa mnadarasa?pia naweza kukipata kitabu?mimi samson toka arusha0786912960 samsnsanya127@gmail.com
ReplyDeleteKwakweli nimependa elimu yenu je mtu akitaka kujifunza zaidi huwa mnadarasa?pia naweza kukipata kitabu?mimi samson toka arusha0786912960 samsnsanya127@gmail.com
ReplyDeletekwa anayehitaji asali nina kiasisi kikubwa cha asali na nta no 0756428695
ReplyDeleteMsaada wa kitabu. Mungu awabariki sana
ReplyDeleteMimi niko moshi mjini na ningependa kufuga naomba kama kuna mawakala wenu hapa ili niweze pata mizinga ya kisasa.
ReplyDeleteAsante
Nimeanza ufugaji nyuki. Hadi Sasa Nina mizinga 85 ya kisasa.mzinga mmoja TU ndio umeingia nyuki tangia Oct/2021. Naomba ushauri.nafugia wilaya ya ulanga kata ya Lupilo. Halmashauri Haina mtaalamu was nyuki
ReplyDeleteKwa wafugaji walioko dodoma wanaweza kuvuna asali zaidi ya maramoja? Kama ndio ni mara ngapi na kipindi kipi na kipi
ReplyDeleteHaiqezekani hate Maria nne kama mzinga yako iko maeneo yanayokua na majimaji kwa mwaka mzima n.a. malisho toshelevu ya Nyuki.
ReplyDeleteNahitaji Kitabu Cha Ufugaji Nyuki na Ushauri Zaidi.
ReplyDeleteWhatsapp Namba-0652380737